Pages

NASH MC.

Thursday, September 12, 2013

JE NASH EMCEE ANAIZUNGUMZIAJE MITINDO HURU?
Ndugu wadau,wakereketwa au wanunuzi wa kazi zetu za HIPHOP na wote wanaotoa mchango wa hali na mali katika kuhakikisha gurudumu la sanaa hii linateleza kama tutakavyoona inafaa..
Leo katika blogu yetu hii ndugu wasomaji na wadau wake tuna kijimada hapo kama kinavyosomeka hapo juu...
Nash Emcee alipata fursa ya kuzungumzia jambo hili ambalo limeonekana kukanganya mbongo za sisi wafatiliaji kwa kujua kuwa mitindo huru au FREE STYLES ni katika nguzo za HIPHOP hivyo sasa Nash anajaribu elezea suala hili kama inavyoonekana hapa chini,karibu....
"Bongo (Tanzania)watu wamejaribu kuingiza mitindo huru kama nguzo ya Hiphop,hakuna freestyle ''mitindo huru'' kama nguzo ya HipHop lazima uwe unajua kughani ndipo uweze kufanya mitindo huru,hiyo ni kama binzari (kinogeshaji)tu katika ughanaji"
Katika hali halisi tu,hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kufanya mitindo huru ya HipHop bila kughani.Mitindo huru ni moja kati ya vipande/kijisehemu kinachounda nguzo ya ughanaji(EMCEEING)....
Ndugu msomaji katika hili na katika kile kinachosisitizwa kuwa Mwanahiphop anahitaji tafuta maarifa (knowledge) katika mambo mbalimbali yanayomzunguka hata pia katika utamaduni wake,natumai ntakua nimejaribu rahisiha hilo katika kupeana maarifa,Amani Kwenu.
(shukrani_(REJEA,Hanzi,M.S,Chuo Kikuu Cha HipHop(2012),Ubunifu Wetu Printing Press,Dar Es Salaam.

No comments:

Post a Comment