Pages

NASH MC.

Tuesday, September 24, 2013

KWANINI NASH ALIJIITA ''MC''?,NANI ''MC'' WA KWANZA,NA NI NANI ALIANZA TUMIA NENO ''MC'' KATIKA HIPHOP?
Naam! sikufikiri na sikudhani kama nilikuwa mwenye makosa makubwa pale nilipokumbuka kuwa mimi ni miongoni mwa watu wenye kuutakia mema utamaduni huu wa HIPHOP kila kukicha kwa kadri nilivyojaaliwa,lakini kutokujuta kwangu moja kwa moja nikiwa nimejiegesha katika kikochi na sauti ya wastani ya ghani mahiri toka kwa wachenguaji bora walionifanya nigeuke teja wa kusikiliza iliingia katika ngoma za masikio yangu.
Vibao vyao na mitambao yao vyote viliendelea chakatwa na ubongo wangu vyema na moja kwa moja vikanisanisafirisha mpaka kwenye kitabu maridhawa kabisa kuhusu utamaduni huu wa HIPHOP nikapenyeza kidole na kwenda kubisha hodi kwenye ukurasa ulioandikwa yaliyomo nao moja kwa moja ukanielekeza ukurasa wa 47 ambapo nilijazwa unene wa maarifa nilipogundua kuwa kilichozungumzwa hapo ni NGUZO ZA HIPHOP,ambapo hapo wengi walijimwaya na kutaja idadi ya NGUZO ZA HIPHOP mfano,
TOVUTI YA URBAN DICTIONARY Ilitoa idadi ya nguzo kama tisa (9)kwa idadi yake kama Mcing,d-jaying,battlelling,graffiti,B-boying,Beat boxing,The style(fashion),The slang,rope skipping,pia hawa hawakubaki nyuma.
WIKIPEDIA. Mtandao huu ulitoa hizi Mcing,d-jaying,break dance,na graffiti,beat boxing,lakini katika hizi Mwanaharakati AFRIKA BAMBATAA alizitaja zote kasoro beat boxing,sasa nkajiuliza JE KUNA NGUZO NGAPI ZA UTAMADUNI HUU?
YOUTH ETHICS INITIATIVE INC kwa ushirikiano na CHUO KIKUU CHA MIAMI. Walisema kiasilia kulikuwa na nguzo nne (4) yaani Uchenguaji,umanju,uvunjaji,machata lakini nguzo ya tano ''Maarifa''ikaongezeka
Swadkta kabisa kuangalia muda nikiwa safari nilijikuta nkigonga mlango (ukurasa) nambari 48 palipodadavuvuliwa nguzo ya maarifa kwa heshima kabisa nikaisoma na kuhitimisha katika kutafuta mengi pitia vyanzo mbalimbali nikazidi ingia ndani ya milango hiyo nikajikuta nikigonga mlango nambari 54,56 na 58.na kuwaleteeni haya.
NANI ALIKUWA ''MC'' WA KWANZA? Ni swali zuri lakini wengi tunaopenda HipHop hatufahamu kama ni kweli,narudi palepele kwamba tafuta ufahamu/maarifa (Knowledge)kama mimi ninavyojaribu pindi panapopatikana upenyo ama muda,safi jibu la swali ni kwamba ingawa inaaminika kuwa COKE LA ROCK ndiye aliyekuwa mchenguaji wa kwanza wa HIPHOP lakini si wa kwanza kuanzisha neno ''MC''sasa.
JE NANI ALIANZA TUMIA NENO HIPHOP? Ndiyo,swali mezani kama tulivyoona hapo juu kuwa Bw.Coke La Rock ndiye mgahanaji wa kwanza lakini hakulitumia neno ''MC''katika kujiita na kuliingiza katika utamaduni wa HipHop kwa kina lakini MELLE MEL huyu anageuka kinara wakuliingiza neno hili katika Hiphop,ndugu huyu aliyezaliwa huko South Bronx jijini New York,Marekani mwaka 1961,alileta athari kubwa katika utamaduni wa HIPHOP kwa kuleta mitindo mbalimbali ya ghani,Mchenguaji wa HipHop wa kwanza kupata tunzo ya Grammy,pia kibao chake kiitwacho ''The Message'' ndicho cha kwanza katika utamaduni wa HipHop kuingia katika kumbukumbu za taifa za vibao vya kihistoria (United States National Archive of Historic Recordings),toka katika hili ndipo laja hili.
JE KWANINI NASH ALIJIITA ''MC''? Katika tafsiri zoefu neno ''Mc'' ni mchenguaji au mshereheshaji au kwa kimombo yaweza andikwa kama ''Master of ceremony''kwa maana ya kuwa muongoza hafla ama sherehe au tumbuizo,akhsante sidhani kama nimetukana katika hili lakini naamini kuwa majina yetu mengi tumerithi kwa wale tulowakuta kwa lengo la kuwaenzi au mapenzi yetu,hivyo kama mistari kadhaa hapo juu ilivyoeleza kuwa MELLE MEL ameacha athari ya mitambao mingi kwa wale waliomfatilia/mashabiki wake hivyo hata jina au neno ''MC'' limekuwa chachu kwa Wanahiphop wengi kujiita mfano,leo tuna NASH MC,P THE MC na wengine wengi pia,lakini athari hizi haziishii tu katika majina bali athari kwa Waghanaji wengi wanaomkubali na kumuelewa Melle Mel,mfano hapa.
Nash MC anasema ''Melle Mel ni mtu wa kwanza kudondosha mistari mitamu,ule utamu wa mistari umeanzia kwa huyu mtu''. Hivyo sasa nakumbuka usemi usemao mwisho wa kizuri cha leo ni mwanzo wa kizuri cha kesho,ndugu zangu katika utamaduni huu naomba niwaache mkiperuzi haa machache niliyowaandaleni,AMANI KWENU. (shukrani,(REJEA,Hanzi,M.S,Chuo Kikuu Cha HipHop(2012),Ubunifu Wetu Printing Press,Dar Es Salaam)uk,54,56 na 58. WAKO,Amri Mlela/Niite Maalim (0654 30 40 30).

No comments:

Post a Comment