Pages

NASH MC.

Wednesday, April 15, 2015

NASH MC: "ZIARA YA KINASA BADO INAENDELEA".

Nash Mc rakabu Zuzu au Maalim Nash ni miongoni mwa wachenguaji mahiri sana nchini Tanzania akiwakilisha sanaa ya muziki kupitia ghani au kemo zake katika utamaduni wa Hiphop, kwa muda mrefu amekuwa ni mtu asiyekata tamaa katika sanaa yake kutokana na vikwazo mbalimbali akutanavyo ambavyo mara nyingi vimekuwa vikimjenga kiubunifu na kufanya makundi mengi kama vijana, wazee, wanawake katika nyadhifa mbalimbali kumpenda na kumuunga mkono katika ununuzi wa kazi zake.

Nash Mc alifanikiwa kufanya onyesho moja jijini Dar es Salaam na kufana vyema, onyesho lilijumuisha wasanii wengi wakiwemo P the Mc, Zaiid na wengine wengi toka jijini hapo vilevile ili kukamilisha maudhui ya tumbuizo hilo " KINASA# NashMcTemekeShow " alikuwepo Mzee. One Sigala toka BAKITA pamoja na waalikwa mbalimbali waliohudhuria siku hiyo.

Ilikuwa ni tukio la aina yake kwa wale walioweza fika kuunga mkono harakati hiyo, ziara ya KINASA bado inaendelea kwa maandalizi ya maonesho mengine mengi nchini Tanzania, ila unajua nini maana ya KINASA?,hujachelewa wewe mpenda sanaa, mpenda Hiphop, shabiki nambari moja wa Nash Mc, Santuri ya onesho lililopita imeshatoka pata nakala yako kuunga mkono harakati. Piga nambari zifuatazo kwa mahitaji +255 713 900 994 au +756 522 346. Amani kwenu.

No comments:

Post a Comment